Thursday, 3 November 2016

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTEUZI WA AWAMU YA NNE, UHAMISHO NA KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) NA STASHAHADA (DIPLOMA) KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwaarifu Waombaji wote walioomba kudahiliwa katika kozi za Astashahada (Cheti) na Stashahada (Diploma) na Umma kwa ujumla kuwa dirisha la maombi lilifungwa mnamo tarehe 15 Oktoba 2016 ili kuruhusu uteuzi wa awamu ya nne kwa waombaji wa kozi hizo. Uteuzi wa awamu ya nne kwa waombaji wa Astashahada na Stashahada unatarajiwa kutangazwa mnamo tarehe 2 Novemba 2016, hivyo basi waombaji wanaombwa kuwa na subira ili kutoa muda kwa Baraza kukamilisha taratibu za uteuzi huo. Maombi mapya ya...
Share:

Wednesday, 2 November 2016

Mke wa Lema aunganishwa kesi ya kumtusi RC Arusha

MKE wa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, Neema Lema (33) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na kuunganishwa katika kesi ya mume wake ya kumtukana Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo kuwa ni shoga. Akimsomea mashitaka hayo kwa mara ya kwanza, Wakili wa Serikali, Blandina Msawa mbele ya Hakimu Augustino Rwezile, alidai kuwa kati ya Agosti 20, mwaka huu ndani ya Arusha, Neema ambaye ni mkazi wa Njiro alimtumia ujumbe wa simu ya kiganjani mkuu huyo wa mkoa wenye lugha ya matusi, huku akijua ni kosa kisheria. Alidai...
Share:

DC ataka Mwalimu Mkuu Mwananyamala kushushwa cheo

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli kumshusha cheo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwananyamala B, Emmanuel Temba kwa makosa mbalimbali, ikiwemo kufanya biashara shuleni. Akitoa agizo hilo katika ziara ya kutembelea kata za manispaa hiyo jana, Hapi alisema ametoa adhabu hiyo kwa kosa la kufanya biashara ya vibanda shuleni hapo wakati agizo la serikali lililotolewa mwaka 2006, haliruhusu biashara shuleni. ‘’Huyu mwalimu mkuu wa shule hii, hatufai haiwezekani afanye biashara ...
Share:

Watumishi changamkieni ununuzi wa nyumba-RC

WATUMISHI wa umma wameshauriwa kuchangamkia fursa ya kununua nyumba zilizojengwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA) kabla ya muda wa kustaafu ili kujitengenezea maisha mazuri baada ya kustaafu. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wakati alipotembelea nyumba za watumishi zilizojengwa na Wakala wa Majengo (TBA) zilizopo eneo la Bunju na nyumba za wananchi Magomeni Kota. Makonda alisema watumishi...
Share:

Tanzania yaipa somo ICC kukabili mpasuko

WAKATI nchi kadhaa za Afrika zikionesha dalili za kutaka kujiengua kutoka Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), Tanzania imeishauri mahakama hiyo kukaa meza moja na nchi wanachama wa Mkataba wa Roma, hasa za Afrika ili kutafuta suluhu ya changamoto na tofauti zilizopo kati ya mahakama hiyo na wanachama wake. Imetoa mwito huo mwanzoni mwa wiki hii kupitia Mwakilishi wake wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa (UN), Balozi Tuvako Manongi wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipopokea na kujadili taarifa ya utendaji wa ICC. Alisema...
Share:

Shein ahimiza mikutano ya watendaji kutatua kero

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein ameeleza umuhimu wa viongozi katika Ofisi na Idara za Serikali kuwa na utaratibu wa kufanya mikutano mara kwa mara na watendaji wao ili kuzungumza na kujadili masuala yao ya kazi. Dk Shein aliyasema kuwa hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kujua matatizo ya watendaji wao pamoja na kukaa kwa pamoja kwa lengo la kujadili na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizopo...
Share:

Songwe wakamata mbegu feki za mahindi

POLISI katika Mkoa wa Songwe wamekamata kilogramu 455 za mbegu zinazoaminika kuwa feki za mahindi katika msako mkali unaoendelea kwa ushirikiano na Kampuni ya Mbegu ya Pana. Kadhalika, watu watano wanashikiliwa na Polisi kutokana na kujihusisha na biashara hiyo ya kuuza mbegu hizo na uchunguzi dhidi yao unaendelea kufanyika. Miongoni mwa maeneo ambayo msako umeendeshwa ni Mji Mdogo wa Mlowo wilayani Mbozi ambako ndiko zimekamatwa mbegu...
Share:

Uvuvi haramu ‘huyeyusha’ matumbawe

MAKAMU wa Rais mstaafu, Dk Mohammed Gharib Bilal ameonya kuwa uvuvi wa haramu unaofanywa na wavuvi katika maeneo ya pwani ya bahari ya Hindi unatishia kutoweka kwa matumbawe, jambo ambalo lina madhara makubwa ya kimazingira kwa nchi. Akitoa mhadhara katika kongamano la mazingira na mabadiliko ya tabianchi lililoandaliwa na kigoda cha Mwalimu Nyerere cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Bilal alisema kitendo cha kuendesha uvuvi haramu kunaharibu...
Share:

Mashali kuagwa Leaders leo

MWILI wa bondia wa ndondi za kulipwa nchini, Thomas Mashali aliyeuawa Kimara jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Jumatatu, utazikwa leo kwenye makaburi ya Kinondoni. Baba mzazi wa marehemu, Malifedha Mashali alisema kuwa mwili wa mtoto wake huyo aliyeuawa kwa kupigwa na watu wasiojulikana, utazikwa katika makaburi ya Kinondoni Mwembejini. Alisema mipango mingine ya mahali utakapoagiwa mwili huo na utakapoombewa, bado ilikuwa inaendelea...
Share:

MNH wakusanya bil 4.6/- kwa mwezi

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) imekuwa ikikusanya mapato ya Sh bilioni 4.6 kwa mwezi kuanzia Desemba mwaka jana hadi kufikia Oktoba mwaka huu, ikiwa ni ongezeko la asilimia 100. Fedha ni zaidi ya wastani wa Sh bilioni 2.3 ilizokuwa ikizalishwa na hospitali hiyo kwa kipindi kama hicho kuanzia Dasemba 2014 hadi Oktoba 2015. Sambamba na ongezeko hilo, pia huduma za vipimo vya MRI, CT –Scan, X-Ray na Ultra Sound zimeongezeka ambapo katika kipindi cha mwaka mmoja sasa, jumla ya wagonjwa waliopimwa kwa kutumia vipimo hivyo wamefikia 55,073...
Share:

Serikali kutumia trilioni 32.9/- mwaka 2017/2018

SERIKALI imepanga kutumia Sh trilioni 32.946 katika bajeti yake ya mwaka 2017/2018, ikiwa imeongezeka kutoka Sh trilioni 29.5 ya mwaka 2016/2017 na kutaja maeneo ya kipaumbele kuwa ni pamoja na kuzingatia miradi ya kufufua kiwanda cha General Tyre cha Arusha na kuendeleza maeneo ya viwanda vidogo. Sambamba na hilo, serikali imebainisha mikakati yake ya kudhibiti matumizi, ambapo sasa itahakikisha mikataba inayoingiwa na serikali na taasisi...
Share:

Vyuo vikuu 15 kitanzini

SERIKALI imetoa siku mbili kwa vyuo vikuu 15, kuwasilisha matokeo ya mitihani kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ya wanafunzi wanufaika na mikopo wanaoendelea na masomo ili kupangiwa mikopo kwa mwaka wa 2016/2017. Vyuo hivyo vilivyokuwa viwasilishe matokeo hayo siku 30 kabla ya kufunguliwa, vimepewa siku hizo kuanzia jana, kabla serikali haijachukua hatua zozote. Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Maimuna...
Share:

Wapinzani wapinga takwimu ukuaji uchumi

LICHA ya takwimu za hivi karibuni kuonesha uchumi wa Taifa pamoja na Pato la Taifa vimekuwa vikikua kwa kasi na kuifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye uchumi imara, kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imedai kuwa uchumi wa Tanzania umeyumba. Kambi hiyo imetaja baadhi ya maeneo yanayothibitisha hilo kuwa ni mikopo inayotolewa na benki za biashara kwenye sekta binafsi kuwa imeshuka katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016. Waziri Kivuli wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Halima Mdee alisema mikopo hiyo imefikia Sh bilioni 1,167.2 ikilinganishwa na...
Share:

Lowassa aongoza vigogo Chadema kuzuru bungeni

VIONGOZI wa juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akiwemo aliyekuwa mgombea wa urais wa chama hicho, Edward Lowassa jana walitembelea bungeni mjini hapa. Lowassa ambaye pia amewahi kuwa Waziri Mkuu, alifika jana saa 2:40 katika viwanja vya Bunge na kutumia dakika kadhaa kusalimiana na baadhi ya wabunge nje ya ukumbi kabla hajaingia ndani. Alipoulizwa na gazeti hili kuhusu ujio wake bungeni, Lowassa, aliyekuwa Mbunge wa Monduli kwa tiketi ya CCM kwa takribani miaka 20 hadi...
Share:

Thursday, 27 October 2016

MATOKEO YA DARASA LA VII TANZANIA 2016

FUNGU HAPA KUPATA MATOK...
Share:

MATOKEO YA DARASA LA VII MKOA WA SHINYANGA

BONYEZA HAPA KUPATA MATOKEO YA DARASA LA VII 20...
Share:

UTOAJI WA MIKOPO KWA WANAFUNZI MWAKA 2016/2017

Baada ya kukamilisha zoezi la Uchambuzi wa maombi ya Mikopo 88,163 yaliyopokelewa hadi kufikia tarehe 11 Agosti, 2016. Jumla ya Wanafunzi wapya 20,183 wamepangiwa Mikopo. Upangaji huu umezingatia vigezo vilivyomo katika mwongozo wa  utoaji wa mikopo uliopitishwa na Bodi ya wakurgezi na kuidhinishwa na wizaya ya elimu sayannsi na teknoloji. Vigezo hivyo ni pamoja na:  I. Vipaumbele vya  kitaifa vinavyoendana na Mpango  wa Maendeleo  wa Taifa wa Miaka mitano, Dira ya Taifa ya  Maendeleo 2025 na Mafunzo...
Share:

Majibu ya Meya Kinondoni kwa wanaohoji uwepo wa Dk. Tulia na Ndalichako

October 23 2016 baraza la halmashauri ya manispaa ya Kinondoni, Dar es salaam lilitangaza ushindi wa nafasi ya umeya kwa Benjamin Sitta ambaye alipigiwa kura na baadhi ya wajumbe. Lakini moja ya headline zilizochukua nafasi kubwa kuanzia kwanye mitandao ya kijamii hadi magazetini ni uhalali wa uchaguzi huo kuwa haukuwa wa haki baada ya kuonekana ushiriki wa Naibu spika Dk. Tulia pamoja na Waziri Ndalichako.   meya huyo ambaye anashare...
Share:

Baada ya Mchungaji Lwakatare kuwatoa wafungwa DSM, sasa ni zamu ya Dodoma

Ikiwa siku kadhaa zimepita tangu Mchungaji wa Kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni B, Dk. Getrude Lwakatare kutoa milioni 25 kwa ajili ya kuwalipia wafungwa 78 ambao walikosa fedha za kulipia faini na kufungwa jela mkoa wa Dar es salaam.  Sasa amejitolea kuwalipia faini wafungwa 50 walioko kwenye magereza mkoani DODOMA, wakiwemo wanaonyonyesha, wazee na watoto. Akizungumza na Ayo Tv na millardayo.com, Lwakatare amesema...
Share:

Mabadiliko ya Yanga na Simba yapigwa stop na serikali

Serikali imezipiga stop klabu za Yanga na Simba kuendelea na michakato yao ya kubadili umiliki wake hadi pale yatakapofanyika marekebisho ya katiba zao. Hayo yalitangazwa jana na Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohamed Kiganja alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Hivi karibuni klabu hizo kongwe ziliazimia kuingia kwenye mabadiliko, Yanga ikikodishwa na mwenyekiti wake Yusuf Manji na Simba ikitaka...
Share:

Model anayedaiwa kutoka kimapenzi na Wema na kudai hamjui Idris Sultan anyoosha maelezo

Wiki moja iliyopita kupitia kipindi kimoja cha runinga, model huyo alisema hamjui Idris Sultan. Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Calisah alisema ni kweli kwamba hamjui Idris Sultan na wala hakuongea kwa nia mbaya au kutafuta kiki. “Mimi nashangaa kwanini watu wamepanic kisa kusema simjui Idris Sultan, kwani yeye ni nani kila mtu amjue?,” aliuliza Model huyo. “Wewe kuna wanamichezo wangapi wameshachukua tuzo kubwa duniani hawajui?. Kwahiyo mimi...
Share:

Dayna Nyange: Lebo yoyote itakayokubali masharti yangu nitafanya nayo kazi

Hitmaker huyo wa ‘Komela’ amemuambia mtangazaji wa Maisha FM ya Dodoma, Silver Touchez “Kikubwa nachoangalia ni sababu, kabla sijajiunga na lebo yoyote lazima niwe na vitu vyangu ambavyo navitaka na wao wanavitu vyao wanavyotaka.” “Record label ni studio tu ambao watu watakuwa wanasimamia kazi zangu ni kitu ambacho mimi mwenyewe ninaweza nikaenda sehemu yoyote nikafanya kazi zangu. Kuna vitu vingi sana kabla hujaingia kwenye lebo yoyote kama...
Share:

Man Utd kukutana na West Ham robo fainali EFL Cup

Mechi za robo fainali EFL Cup ratiba imetoka baada ya kumuondoa Guardiola, Mourinho sasa atacheza na Bilic. Mechi hizi zitachezwa katika wiki inayoanza Tarehe 28,Novemba. Hii ndo ratiba kamili ya Michuano ya EFL Cup. ...
Share:

‘Magufuli ameletea msiba Dodoma’

WAKATI serikali ya awamu ya tano ikiendelea na hekaheka za kuhamishia makao makuu yake mkoani Dodoma, baadhi ya wakazi wa mkoa huo wamelaani hatua hiyo ya serikali na kusema inawasababishia matatizo makubwa, Wakizungumza na mtandao huu, wakazi wa Ndachi kata ya Miyuji, Manispaa ya Dodoma, wamesema baada ya serikali kutangaza kuhamishia makao makuu yake Dodoma, tayari wameanza kuporwa ardhi yao. Wameenda mbali zaidi na kutishia kuwakata...
Share:

RC MWANZA APOKEA UJUMBE WA WAWEKEZAJI KUTOKA KOREA.

Awaahidi ushirikiano. Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amepokea ujumbe wa wawekezaji kutoka nchini Korea Kusini, wenye niya yakuwekeza katika mkoa wa Mwanza ukiwa na ujumbe wa watu kumi na watano nakufanya nao mazungumzo mapema katika Ofisi yake kabla yakuendelea na ziara yao katika Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela. Katika mazungumzo yao yaliyodumu saa 1:33, Mkuu wa Mkoa amewahakikishia utayari wa mkoa wa Mwanza kuwapokea wawekezaji kutoka nchini humo lakini pia kuwabainishia maeneo mbali mbali katika sekta ya...
Share:

RC MWANZA ATOA SOMO KWA WAREMBO MISS TANZANIA. 2016

MKUU wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, amewaasa warembo wanaoshiriki shindano la Mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania-2016), kutambua wana jukumu zito mbele yao la kuzisaidia jamii zao katika majukumu mbali mbali ya kijamii. Mongella alitoa kauli hiyo muda mfupi mara baada ya warembo 30 wanaoshiriki shindano hilo kumtembelea ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha. Mongella aliwataka warembo hao kufanyakazi kwa bidii na kujituma kwani ndio njia pekee itakayowawezesha kuondokana na umasikini. “Jijengeeni tabia...
Share:

Ofisa usalama feki atupwa jela miaka 2

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala imemhukumu Seleman Manoti, kifungo cha miaka miwili jela kwa kupatikana na hatia ya kujifanya usalama wa Taifa. Hata hivyo, mahakama imetoa hukumu hiyo bila mshitakiwa kuwepo mahakamani kutokana na kuruka dhamana kesi hiyo ilipokuwa inasikilizwa. Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi, Flora Haule alisema kuwa upande wa mashitaka, ulileta mashahidi wanne kwa ajili ya kuthibitisha tuhuma hizo. Alisema kutokana na ushahidi uliotolewa, mahakama imeridhishwa na ushahidi huo na kwamba mahakama inamtia hatiani mshitakiwa...
Share:

TFS yanasa lori lenye shehena ya mbao

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wamekamata lori lililokuwa likisafirisha mbao zilizovunwa kinyume cha sheria baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria. Lori hilo lenye namba za usajili T 676ANQ aina ya Scania lililokuwa likitoka Kigoma kwenda jijini Dar es Salaam, lilikutwa limetelekezwa katika maegesho ya mkazi wa Dar es Salaam, eneo la Amana katika Manispaa ya Ilala na dereva wa lori hilo kutokomea kusikojulikana. Hata hivyo,...
Share:

Kiini cha nauli juu Dar-Zanzibar chaelezwa

TATIZO la uhaba wa vyombo vya usafiri kati ya Zanzibar na Tanzania Bara ikiwemo boti zinazokwenda kwa kasi, kwa kiasi kikubwa kumechangia kuwepo kwa tatizo la ulanguzi wa tiketi kwa abiria na kusababisha usumbufu mkubwa. Ulanguzi wa tiketi hizo umeshuhudiwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Ujenzi na Uchukuzi, Mohammed Ahmada wakati alipofanya ziara katika eneo la bandari ya Malindi. Tiketi moja ya boti zinazokwenda kwa kasi zinazomilikiwa...
Share:

Serikali yazindua mpango maalumu kuboresha afya

SERIKALI imezindua mpango maalumu kitaifa wa kuboresha afya ujulikanao kama Mkoba wa siku 1,000 utakaotumika kutekeleza afua mbalimbali za lishe nchini kwa lengo la kupunguza udumavu kwa watoto na upungufu wa damu kwa wajawazito na wanyonyeshao. Mkoba wa siku 1,000 ni nyenzo ya uwezeshaji unaotumia njia mbalimbali za mawasiliano yenye lengo la kushawishi mabadiliko ya tabia na mitazamo kuhusu lishe katika jamii, ukihamasisha wajibu wa kijinsia wa wazazi na walezi walio ndani ya siku 1,000 za mwanzo wa maisha ya mwanadamu ambazo zinahesabiwa...
Share:

Wanaosomea fani za kipaumbele wapewe mikataba

TAARIFA kwamba serikali inakusudia kuweka utaratibu wa kuwabana wanafunzi wanaopewa mikopo katika fani za kipaumbele, kutumikia utumishi wa umma kwa muda fulani, haina budi kuungwa mkono na kila mpenda maendeleo ya kweli. Fani ambazo serikali kwa makusudi imezipa kipaumbele kwa lengo la kupata wataalamu wa kutosha katika maeneo husika, ambayo kwa sasa yana wataalamu wachache ni pamoja na fani za sayansi ya tiba na afya, ualimu wa sayansi na hisabati, uhandisi wa viwanda, kilimo, mifugo, mafuta, gesi asilia, sayansi asilia, mabadiliko...
Share:

Polisi yawashikilia wanne mtandao wizi wa magari

POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam inawashikilia watu wanne kwa tuhuma za wizi wa magari kwa kununua nyaraka za magari yaliyopata ajali na kulipwa na bima. Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Kamishna wa Polisi, Simon Sirro alisema jana Dar es Salaam kuwa askari waliwakamata watuhumiwa hao baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema. “Watuhumiwa hawa wanajihusisha na wizi wa magari kwa mbinu ya kununua nyaraka za magari yaliyopata ajali...
Share:

Pluijm aziita timu zinazomtaka

KOCHA Hans van Pluijm amesema milango iko wazi kwa timu yoyote inayomhitaji. Kocha huyo Mholanzi alitangaza kujiuzulu juzi baada ya waajiri wake Yanga kuingia mkataba na kocha wa Zesco ya Zambia, George Lwandamina bila kumshirikisha. Akizungumza na gazeti hili jana, Pluijm alikiri timu kadhaa kumwania lakini akasema ni mapema kuzitaja na kusisitiza amefungua milango kwa yeyote inayomtaka kumfuata kwa mazungumzo. “Muhimu siwezi kukaa bila...
Share:

Serikali yazipiga stop Yanga, Simba

SERIKALI imezipiga stop klabu za Yanga na Simba kuendelea na michakato yao ya kubadili umiliki wake hadi pale yatakapofanyika marekebisho ya katiba zao. Hayo yalitangazwa jana na Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohamed Kiganja alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Hivi karibuni klabu hizo kongwe ziliazimia kuingia kwenye mabadiliko, Yanga ikikodishwa na mwenyekiti wake Yusuf Manji na Simba ikitaka...
Share:

Mbarawa awataka Posta kukusanya mapato

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amewataka wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Posta Tanzania kusimamia mapato kwa kukusanya fedha kinyume cha hapo atachomoa mmoja mmoja na kuweka wengine kwa nusu saa tu. Aliyasema hayo jana alipokuwa akizindua Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo jijini Dar es Salaam. Katika uzinduzi huo, alisema kwa kuwa serikali inahitaji fedha, kama waziri hahitaji kuambiwa maneno...
Share:

Historia MOI upasuaji kwa wenye kibiongo

KIBIONGO ni tatizo la kupinda kwa mgongo upande moja hasa wa kulia, hali inayomfanya mtu aliye na hali hiyo kutembea akiwa ama ameinama au kujikunja. Tatizo hilo mtu huweza kuzaliwa nalo au kutokea baadaye mtoto anapokuwa amefikisha umri wa miaka mitatu na kuendelea. Kwa kuwa hapa nchini kulikuwa hakuna upasuaji kwa tatizo hilo, watu waliokuwa na shida hiyo walikuwa wakikua nalo hivyo hivyo isipokuwa wenye uwezo wa kifedha na kuwa na taarifa sahihi walipelekwa nje ya nchi kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji. Hivi sasa ufumbuzi umepatikana...
Share:

Mfumo wa PReM utakavyodhibiti wanafunzi hewa

TANGU serikali iliporuhusu mazingira ya soko huria katika sekta ya elimu, kumekuwapo na shule binafsi nyingi. Katika shule hizo binafsi, suala la kuhamisha wanafunzi limekuwa halizingatiwi kama ilivyokuwa miaka ya nyumba ambapo ilikuwa ni lazima taarifa za mwanafunzi za kuhama zipate baraka na mamlaka za elimu katika ngazi za kata, wilaya na mkoa na taarifa kubaki katika ngazi hizo. Kukatika kwa mnyororo huo ulifanywa uhamishaji na taarifa...
Share:

Yanga siku 5 bao kumi

ANGA siku tano bao 10! ndivyo ilivyotokea jana baada ya mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu kushinda mabao 4-0 dhidi ya JKT Ruvu na hivyo kuwa na mabao 10 ndani ya siku tano baada ya kuifunga Kagera Sugar mabao 6-2 Jumamosi iliyopita. Ushindi huo uliopatikana kwenye uwanja wa Uhuru Dar es Salaam umeifanya Yanga kuendelea kushika nafasi ya pili kwenye msimamo ikiwa na pointi 24, tofauti ya pointi tano na vinara wa ligi hiyo, Simba. Katika ...
Share:

Kagera yatumia mil. 800/- ukarabati miundombinu

UKARABATI wa miundombinu iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi mkoani Kagera umeanza, na tayari Sh milioni 800 zimetumika kati ya Sh bilioni tano zilizotolewa na wadau mbalimbali katika kuwachangia waathirika wa tetemeko hilo lililotokea Sept 10, mwaka huu na kusababisha vifo, uharibifu wa majengo na miundombinu mbalimbali. Aidha, imeelezwa kuwa, inahitaji miaka miwili au mitatu kwa mkoa huo kurejea katika hali ya kawaida kutokana na maeneo...
Share:

nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba

nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba