Friday, 12 August 2016

Magufuli ‘azika’ demokrasia

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania, ameonesha wazi dhamira ya kuzuia mikutano na maandamano ya vyama vya siasa nchini katika kipindi cha utawala wake wa miaka mitano, anaandika Moses Mseti. Julai 26 mwaka huu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kilitangaza kufanya mikutano ya hadhara nchini chini ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho. Chadema kilitangaza Oparesheni ya Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) kwa kile...
Share:

Serikali: Hatuna ushahidi wa kuzihukumu shule za Feza

SERIKALI imesema haina ushahidi wa kutosha kuzitia hatiani shule za Feza nchini zinazodaiwa kumilikiwa na mmoja wa wananchi wa Uturuki anayetuhumiwa kujihusisha na ugaidi na kuitaka Serikali ya Uturuki kuwasilisha taarifa zenye ushahidi wa kutosha kuhusu tuhuma hizo. Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga. Alisema walipokea madai kutoka Ubalozi wa Uturuki nchini kuwa shule hizo zinamilikiwa na mmoja wa wananchi wa nchi hiyo anayejihusisha na ugaidi. Balozi...
Share:

Korti Kuu yarejesha shitaka alilofutiwa Kitilya

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetengua uamuzi wa kufutwa kwa shitaka la utakatishaji fedha linalomkabili aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake na kuamuru kesi hiyo iendelee katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Jaji Edson Mkasimongwa alitoa uamuzi huo jana baada ya kukubali hoja za rufaa ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) na kuamuru kesi hiyo iendelee pale ilipoishia kabla ya kutolewa kwa uamuzi...
Share:

Tanesco, TIB waamriwa kulipa fidia wananchi

NAIBU Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani ameliagiza Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) na benki ya TIB kuhakikisha wanalipa sehemu ya fidia iliyobaki ya Sh bilioni 46 kwa wananchi watakaopitiwa na mradi wa usafirishaji umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Somanga Fungu, Kilwa mkoani Lindi hadi Kinyerezi, Dar es Salaam. Agizo hilo la Dk Kalemani limeelezwa linapaswa kuanza kutekelezwa kuanzia Agosti 17, mwaka huu. Alitoa agizo...
Share:

Wednesday, 10 August 2016

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI KATIKA KOZI ZA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

Baraza linapenda kuwaarifu wote walioomba kudahiliwa katika kozi za cheti na diploma na umma kwa ujumla kuwa muda wa nyongeza wa kutuma maombi kwa mwaka 2016/2017 umeongezwa hadi tarehe 13 Agosti 2016 ili kuruhusu ambao hawakukamilisha maombi yao kuyamaliza na ambao hawajafanikiwa kuomba kutuma maombi yao. Baraza linaomba ifahamike kuwa vyuo na kozi zilizojaa hazitaonekana tena wakati wa maombi bali kozi zitakazoonekana ni zile zenye nafasi...
Share:

Bilionea wa milioni 7/- kwa dakika akwama

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya kufutwa kwa shitaka la utakatishaji fedha katika katika kesi ya kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 14 inayomkabili, mfanyabiashara Mohammed Yusufali ‘Choma’ na mwenzake. Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri alitoa uamuzi huo jana baada ya kupitia hoja zilizowasilishwa na pande zote mbili katika kesi hiyo. Kutokana na uamuzi huo, washitakiwa wataendelea kusota rumande hadi...
Share:

Tuesday, 9 August 2016

Tanzania yaanza vibaya Olimpiki

TANZANIA jana ilianza vibaya Michezo ya 31 ya Olimpiki baada ya mchezaji wake wa judo, Andrew Thomas Mlugu kudundwa na Jake Bensted wa Austria katika mchezo wa kilo 73. Tanzania katika michezo hiyo iliyoanza Agosti 5, imepeleka wachezaji saba, judo akiwa mchezaji mmoja, wawili wa kuogelea, ambao ni Magdalena Moshi na Hilal Hilal na wale wa riadha, ambao bado hawajaenda Rio kutokana na ratiba yao kuwa mwishoni. Mchezaji huyo wa judo alishiriki mashindano hayo kupitia tiketi ya upendeleo baada ya kushindwa kufuzu kwa njia ya kawaida. ...
Share:

Manji kutinga kizimbani leo

MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji leo atapanda kizimbani Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi alikoburuzwa na waliokuwa watendaji wa klabu hiyo, Selestine Mwesigwa na Luis Sendeu. Septemba mwaka 2012, Mwesigwa akiwa Katibu Mkuu wa Yanga na Sendeu akiwa Ofisa Habari wa klabu hiyo ya Jangwani, waliondolewa katika ajira zao kwa kile kilichoelezwa kuwa utendaji mbovu. Mwesigwa na Sendeu waliomba bila mafanikio walipwe na Yanga fidia ya Sh 262 milioni, ambapo kati ya hizo, Sendeu anadai Sh 79 milioni na Mwesigwa anadai Sh 183 milioni. Watendaji...
Share:

Simba yaleta raha

SIMBA jana ilisherehekea vizuri miaka 80 tangu ilipoanzishwa baada ya kuichabanga AFC Leopards ya Kenya mabao 4-0 katika mchezo wa tamasha la `Simba Day’ kwenye Uwanja wa Taifa. Kocha Mkuu wa timu hiyo, Joseph Omog juzi aliwataka wanachama, wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa kushuhudia kikosi kitakachotwaa taji la Tanzania Bara msimu wa mwaka 2016/2017. Simba ilipata bao la kuongoza katika dakika ya...
Share:

Brazil kuwekeza kwenye umeme nchini

SERIKALI ya Brazil imeonesha nia kuwekeza katika sekta ya nishati nchini hususan katika kuzalisha umeme kwa kutumia maji na mabaki ya miwa. Hayo yalielezwa jijini Dar es Salaam jana na Balozi wa Brazil nchini, Carlos Alfonso Puente, alipomtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ofisini kwake na kufanya mazungumzo naye. Balozi Puente alimweleza Profesa Muhongo kuwa nchi yake ina ujuzi na uzoefu wa kutosha katika...
Share:

Mafisadi fedha za miradi kukiona

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ya Awamu ya Tano, itapambana kwa nguvu zote na vitendo vya ufisadi kwenye fedha, zinazoelekezwa kwenye miradi ya maendeleo. Amesema serikali ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kijamii kwa kuendelea kupambana na vitendo vya rushwa na ufisadi, kudhibiti matumizi yasiyo lazima na kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa kodi ili fedha zinazokusanywa, zielekezwe kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi. Alisema hayo jana wakati akifunga maadhimisho ya Sikukuu ya...
Share:

Wakuu wa nchi za EAC waombwa kusimamia amani, utulivu

WAKUU wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC), wameombwa kusimamia amani na utulivu wa kisiasa katika nchi za ukanda huo, kwa lengo la kuweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi kufanya shughuli zake bila matatizo. Ombi hilo lilitolewa juzi na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Afrika Mashariki (EABC), Felix Mosha, alipozungumza na wanahabari, baada ya kumalizika kwa kikao cha Bodi ya baraza hilo jijini hapa. Mosha aliwaomba wakuu wa nchi hizo ikiwemo Sudan Kusini kuhakikisha wanasimamia suala la utulivu wa kisiasa katika nchi zao ili kusaidia...
Share:

Acacia yatoa ushuru wa huduma wa mil 717.2/-

KAMPUNI ya Acacia inayomiliki Mgodi wa dhahabu wa Buzwagi wilayani hapa mkoani Shinyanga, imekabidhi hundi ya Sh milioni 717.2 kwa Halmashauri ya Mji wa Kahama ikiwa ni ushuru wa huduma kwa kipindi cha miezi sita iliyopita. Akikabidhi hundi hiyo mbele ya wananchi wa Mji wa Kahama katika viwanja vya Halmashauri ya Mji huo, Meneja Mkuu wa Mgodi huo, Assa Mwaipopo, alisema kuwa ushuru huo wa huduma unapaswa kulipwa mara mbili kwa mwaka. Mwaipopo...
Share:

Familia 8 zanusurika kufa kwa moto

FAMILIA nane zenye watu zaidi ya 20 kwenye mtaa wa Mharakani kata ya Picha ya Ndege wilayani Kibaha mkoani Pwani zimenusurika kufa baada ya moto kutokea wakati wanafamilia hao wakiwa wamelala. Wakizungumza na mwandishi wa habari hii, waathirika wa tukio hilo la moto walisema lilitokea usiku wa kuamkia Agosti 8, mwaka huu saa 6:30 usiku. Mmoja wa waathirika hao, Emmanuel Mhina, alisema watu waliokuwa jirani na nyumba yao ndio waliowafahamisha juu ya moto huo ambao unasadikiwa ulianzia kwenye moja ya maduka yaliyo kwenye nyumba hiyo. Alisema...
Share:

Uteuzi alioufanya Waziri Nape leo August 09 2016

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE MicrosoftInternetExplorer4 ...
Share:

nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba

nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba