HALI imezidi kuwa tete ndani ya Chama Cha Msalaba Mwekundu Tanzania
(TRCS) baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuzifunga akaunti zaidi
ya nne za chama hicho kutokana na kushindwa kulipa malimbikizo ya kodi
ya makato ya mshahara wa wafanyakazi (PAYE).
Taarifa kutoka ndani ya TRCS zinaeleza kuwa kodi inayodaiwa na TRA ni
ile ya PAYE ya wafanyakazi zaidi 200 wanaofanya kazi mkoani Kigoma
katika kambi za wakimbizi kati ya mwaka 2011/2015.
Kodi hiyo inakadiriwa kufikia shilingi milioni 790 huku chama hicho
kikidaiwa pia shilingi...
Monday, 5 September 2016
MAYANGA ATAMBIA KIKOSI CHAKE
KOCHA wa Mtibwa Sugar Salum Mayanga amesema ushindi walioupata katika
mchezo dhidi ya Majimaji umetokana na juhudi za kuboresha kikosi chake
mara kwa mara pindi wanapobaini mapungufu.
Mtibwa Sugar iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo uliochezwa juzi kwenye Uwanja wa Majimaji,Songea.
Ushindi huo unaifanya Mtibwa Sugar kufikisha pointi sita baada ya
kushinda michezo miwili dhidi ya Ndanda FC mabao 2-1 na Majimaji mabao
2-1 na kufungwa mmoja dhidi ya Ruvu Shooting.
Akizungumza na gazeti hili, Mayanga alisema kikosi chake kilifanikiwa
...
Kiir akubali wanajeshi wa UN watumwe Juba, Sudan Kusini

Rais wa Sudan Kusini hatimaye amekubali kikosi cha ziada cha wanajeshi wa kulinda amani kitumwe nchini humo.
Rais Salva Kiir alichukua hatua hiyo baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Bw
Kiir alikuwa awali amekataa kutumwa kwa wanajeshi hao 4,000 kutoka
mataifa ya kanda, akisema huo ni ukiukaji wa uhuru wa Sudan Kusini.
UN yaidhinisha kuongeza wanajeshi Juba
John Kerry aitaka Sudan Kusini...
TAMWA YAPAMBANA NA AJALI KUOKOA MAISHA
AJALI za barabarani zinaua watu takribani milioni 1.25 duniani kila
mwaka wakati hapa nchini takwimu zinaonesha katika ajali za miezi sita
kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu, watu 1,580 wameshapoteza maisha
kutokana na ajali hizo.
Tawimu zilizotolewa na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani,
Mohamed Mpinga zinaonesha kwamba marehemu hao 1,580 walitokana na ajali
5,152 ambapo watu waliojeruhiwa ni 4,659. Wanawake waliokufa kutokana na
ajali hizo Kamanda Mpinga anasema ni 301.
Kati ya ajali hizo mkoa wa Mbeya ulikuwa unaongoza kwa...
UWANJA WA KARUME PEMBA WAANZA KUTOA HUDUMA
UWANJA wa Ndege wa Karume uliopo Pemba sasa umeanza kutoa huduma za kutua na kuruka kwa ndege nyakati zote ikiwemo usiku.
Hali hiyo inatokana na matengenezo makubwa yaliyofanywa kwa kuweka
taa za kuongoza ndege na zinazoruhusu ndege kutua nyakati za usiku,
mradi unaotajwa kuigharimu Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zaidi ya Sh
bil 1.6.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Issa Haji Ussi (Gavu) alisema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi
zilizochukuliwa na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuona kisiwa
cha...
MAMIA WAUAGA MWILI WA MKURUGENZI WA MAREHEMU A TO Z
MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ameongoza wakazi wa mkoa huo
kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda cha A to Z , Anuj
Shah, cha jijini hapa, kinachotengeneza vyandarua vyenye dawa.
Mwili wa Shah uliagwa jana na wafanyakazi wa kiwanda hicho, majirani
wa kiwanda hicho, pamoja na rafiki zake kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Uliagwa katika makazi yake yaliyopo Kisongo na baadaye kuzikwa kwa kuchomwa moto kwenye makaburi ya Esso jijini hapa.
Akizungumza wakati wa maziko, Gambo alisema Shah alipenda kila
Mtanzania mwenye nguvu...
Thursday, 1 September 2016
JIONEE SIKU YA KUPATWA KWA JUA LEO SEPTEMBA 1, 2016

TUMESHATANGAZIWA kuwa leo kutakuwa na kupatwa kwa jua. Kwa hapa Tanzania tukio hilo litatokea kati ya saa nne asubuhi na saa sita mchana.
Tukio hili ni la kawaida ambapo kivuli cha mwezi kinapokuwa kwenye eneo la dunia. Dunia inapolizunguka jua na mwezi kuzunguka dunia, hutokea mwezi ukakaa katikati ya jua na dunia katika mstari mnyoofu na kuzuia mwanga wa jua kufika duniani. Tukio hili hujulikana kama kupatwa kwa jua. Kwa kanuni za mwanga,...
VITAMBULISHO VYA UTAIFA KUKOMESHA WAHAMIAJI HARAMU KIGOMA

MADIWANI wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, wamelalamikia operesheni ya kukamata wahamiaji haramu inayoendelea mkoani Kigoma na kupendekeza kuwa ili kumaliza tatizo hilo, serikali haina budi kuharakisha utoaji wa vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wa mkoa huo.
Wakizungumza katika mkutano wa kujadili mpango wa Tushirikishane unaosimamiwa na Jamii Forum, baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo, walisema kuwa ukamataji unaofanyika sasa,...
VODACOM YATOA UFAFANUZI ONGEZEKO LA MAPATO
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Vodacom imesema ongezeko la mapato ya Sh bilioni 1.9 halina uhusiano wowote na ufungwaji wa mtambo mpya wa kuratibu mapato ya kampuni ya simu au kodi ambazo hazijalipwa kipindi cha nyuma, bali limetokana na Sheria mpya ya Kodi ya Mwaka 2016.
Aidha, imefafanua kuwa katika kipindi kifupi mabadiliko hayo yataongeza pato la serikali, lakini mabadiliko hayo yanaonesha kwamba matokeo hayo yatapunguza watumiaji wa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi kutokana na watumiaji kutomudu gharama.
Kampuni hiyo ilikuwa ikitoa...
WATUMISHI 15 SIHA WAHOJIWA IKULU
MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha, mkoani Kilimanjaro, Valerian Jual, amesema watumishi 15 wa halmashauri hiyo wanaohojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kutokana na tuhuma mbalimbali.
Jual alitoa taarifa hizo juzi wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadik, aliyetembelea wilaya ya Siha kwa lengo la kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali.
Alisema licha ya watuhumiwa hao, pia watumishi wengine watano walishikiliwa na jeshi la Polisi kwa kukosa dhamana wakituhumiwa...
NINA IMANI NA VIONGOZI WALIOCHAGULIWA KWA HAKI
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) anayemaliza muda wake, ambaye pia ni Rais wa Botswana, Dk Seretse Kahama Ian Khama, amempongeza Rais John Magufuli kwa kuchaguliwa kwake kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka jana.
Rais huyo wa Botswana alitoa pongezi hizo kupitia hotuba aliyoitoa kwenye ufunguzi wa Mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC unaofanyika Mbabane- Swaziland ambako Dk Magufuli anawakilishwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
Dk Khama alisema, ukuaji wa demokrasia katika nchi...
KIDATO CHA 5 AWAMU YA PILI 2016
TAARIFA KWA UMMA
31-AUG-2016.
OR-TAMISEMI inatangaza majina ya
wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano awamu ya Pili
(Second Selection) kwa mwaka 2016. Jumla ya wanafunzi 3,918 wakiwemo
wasichana 2,413 na wavulana 1,505 wamechaguliwa kujiunga na Kidato
cha Tano awamu ya pili kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi na
wanafunzi ambao hawakuripoti awamu ya kwanza.
Kati
ya wanafunzi waliochaguliwa 1,864 wakiwemo wasichana 1,099 na wavulana
765 sawa na asilimia 47.58 watajiunga...