Thursday, 3 November 2016

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTEUZI WA AWAMU YA NNE, UHAMISHO NA KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) NA STASHAHADA (DIPLOMA) KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwaarifu Waombaji wote walioomba kudahiliwa katika kozi za Astashahada (Cheti) na Stashahada (Diploma) na Umma kwa ujumla kuwa dirisha la maombi lilifungwa mnamo tarehe 15 Oktoba 2016 ili kuruhusu uteuzi wa awamu ya nne kwa waombaji wa kozi hizo. Uteuzi wa awamu ya nne kwa waombaji wa Astashahada na Stashahada unatarajiwa kutangazwa mnamo tarehe 2 Novemba 2016, hivyo basi waombaji wanaombwa kuwa na subira ili kutoa muda kwa Baraza kukamilisha taratibu za uteuzi huo. Maombi mapya ya...
Share:

Wednesday, 2 November 2016

Mke wa Lema aunganishwa kesi ya kumtusi RC Arusha

MKE wa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, Neema Lema (33) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na kuunganishwa katika kesi ya mume wake ya kumtukana Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo kuwa ni shoga. Akimsomea mashitaka hayo kwa mara ya kwanza, Wakili wa Serikali, Blandina Msawa mbele ya Hakimu Augustino Rwezile, alidai kuwa kati ya Agosti 20, mwaka huu ndani ya Arusha, Neema ambaye ni mkazi wa Njiro alimtumia ujumbe wa simu ya kiganjani mkuu huyo wa mkoa wenye lugha ya matusi, huku akijua ni kosa kisheria. Alidai...
Share:

DC ataka Mwalimu Mkuu Mwananyamala kushushwa cheo

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli kumshusha cheo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwananyamala B, Emmanuel Temba kwa makosa mbalimbali, ikiwemo kufanya biashara shuleni. Akitoa agizo hilo katika ziara ya kutembelea kata za manispaa hiyo jana, Hapi alisema ametoa adhabu hiyo kwa kosa la kufanya biashara ya vibanda shuleni hapo wakati agizo la serikali lililotolewa mwaka 2006, haliruhusu biashara shuleni. ‘’Huyu mwalimu mkuu wa shule hii, hatufai haiwezekani afanye biashara ...
Share:

Watumishi changamkieni ununuzi wa nyumba-RC

WATUMISHI wa umma wameshauriwa kuchangamkia fursa ya kununua nyumba zilizojengwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA) kabla ya muda wa kustaafu ili kujitengenezea maisha mazuri baada ya kustaafu. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wakati alipotembelea nyumba za watumishi zilizojengwa na Wakala wa Majengo (TBA) zilizopo eneo la Bunju na nyumba za wananchi Magomeni Kota. Makonda alisema watumishi...
Share:

Tanzania yaipa somo ICC kukabili mpasuko

WAKATI nchi kadhaa za Afrika zikionesha dalili za kutaka kujiengua kutoka Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), Tanzania imeishauri mahakama hiyo kukaa meza moja na nchi wanachama wa Mkataba wa Roma, hasa za Afrika ili kutafuta suluhu ya changamoto na tofauti zilizopo kati ya mahakama hiyo na wanachama wake. Imetoa mwito huo mwanzoni mwa wiki hii kupitia Mwakilishi wake wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa (UN), Balozi Tuvako Manongi wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipopokea na kujadili taarifa ya utendaji wa ICC. Alisema...
Share:

Shein ahimiza mikutano ya watendaji kutatua kero

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein ameeleza umuhimu wa viongozi katika Ofisi na Idara za Serikali kuwa na utaratibu wa kufanya mikutano mara kwa mara na watendaji wao ili kuzungumza na kujadili masuala yao ya kazi. Dk Shein aliyasema kuwa hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kujua matatizo ya watendaji wao pamoja na kukaa kwa pamoja kwa lengo la kujadili na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizopo...
Share:

Songwe wakamata mbegu feki za mahindi

POLISI katika Mkoa wa Songwe wamekamata kilogramu 455 za mbegu zinazoaminika kuwa feki za mahindi katika msako mkali unaoendelea kwa ushirikiano na Kampuni ya Mbegu ya Pana. Kadhalika, watu watano wanashikiliwa na Polisi kutokana na kujihusisha na biashara hiyo ya kuuza mbegu hizo na uchunguzi dhidi yao unaendelea kufanyika. Miongoni mwa maeneo ambayo msako umeendeshwa ni Mji Mdogo wa Mlowo wilayani Mbozi ambako ndiko zimekamatwa mbegu...
Share:

Uvuvi haramu ‘huyeyusha’ matumbawe

MAKAMU wa Rais mstaafu, Dk Mohammed Gharib Bilal ameonya kuwa uvuvi wa haramu unaofanywa na wavuvi katika maeneo ya pwani ya bahari ya Hindi unatishia kutoweka kwa matumbawe, jambo ambalo lina madhara makubwa ya kimazingira kwa nchi. Akitoa mhadhara katika kongamano la mazingira na mabadiliko ya tabianchi lililoandaliwa na kigoda cha Mwalimu Nyerere cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Bilal alisema kitendo cha kuendesha uvuvi haramu kunaharibu...
Share:

Mashali kuagwa Leaders leo

MWILI wa bondia wa ndondi za kulipwa nchini, Thomas Mashali aliyeuawa Kimara jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Jumatatu, utazikwa leo kwenye makaburi ya Kinondoni. Baba mzazi wa marehemu, Malifedha Mashali alisema kuwa mwili wa mtoto wake huyo aliyeuawa kwa kupigwa na watu wasiojulikana, utazikwa katika makaburi ya Kinondoni Mwembejini. Alisema mipango mingine ya mahali utakapoagiwa mwili huo na utakapoombewa, bado ilikuwa inaendelea...
Share:

MNH wakusanya bil 4.6/- kwa mwezi

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) imekuwa ikikusanya mapato ya Sh bilioni 4.6 kwa mwezi kuanzia Desemba mwaka jana hadi kufikia Oktoba mwaka huu, ikiwa ni ongezeko la asilimia 100. Fedha ni zaidi ya wastani wa Sh bilioni 2.3 ilizokuwa ikizalishwa na hospitali hiyo kwa kipindi kama hicho kuanzia Dasemba 2014 hadi Oktoba 2015. Sambamba na ongezeko hilo, pia huduma za vipimo vya MRI, CT –Scan, X-Ray na Ultra Sound zimeongezeka ambapo katika kipindi cha mwaka mmoja sasa, jumla ya wagonjwa waliopimwa kwa kutumia vipimo hivyo wamefikia 55,073...
Share:

Serikali kutumia trilioni 32.9/- mwaka 2017/2018

SERIKALI imepanga kutumia Sh trilioni 32.946 katika bajeti yake ya mwaka 2017/2018, ikiwa imeongezeka kutoka Sh trilioni 29.5 ya mwaka 2016/2017 na kutaja maeneo ya kipaumbele kuwa ni pamoja na kuzingatia miradi ya kufufua kiwanda cha General Tyre cha Arusha na kuendeleza maeneo ya viwanda vidogo. Sambamba na hilo, serikali imebainisha mikakati yake ya kudhibiti matumizi, ambapo sasa itahakikisha mikataba inayoingiwa na serikali na taasisi...
Share:

Vyuo vikuu 15 kitanzini

SERIKALI imetoa siku mbili kwa vyuo vikuu 15, kuwasilisha matokeo ya mitihani kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ya wanafunzi wanufaika na mikopo wanaoendelea na masomo ili kupangiwa mikopo kwa mwaka wa 2016/2017. Vyuo hivyo vilivyokuwa viwasilishe matokeo hayo siku 30 kabla ya kufunguliwa, vimepewa siku hizo kuanzia jana, kabla serikali haijachukua hatua zozote. Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Maimuna...
Share:

Wapinzani wapinga takwimu ukuaji uchumi

LICHA ya takwimu za hivi karibuni kuonesha uchumi wa Taifa pamoja na Pato la Taifa vimekuwa vikikua kwa kasi na kuifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye uchumi imara, kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imedai kuwa uchumi wa Tanzania umeyumba. Kambi hiyo imetaja baadhi ya maeneo yanayothibitisha hilo kuwa ni mikopo inayotolewa na benki za biashara kwenye sekta binafsi kuwa imeshuka katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016. Waziri Kivuli wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Halima Mdee alisema mikopo hiyo imefikia Sh bilioni 1,167.2 ikilinganishwa na...
Share:

Lowassa aongoza vigogo Chadema kuzuru bungeni

VIONGOZI wa juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akiwemo aliyekuwa mgombea wa urais wa chama hicho, Edward Lowassa jana walitembelea bungeni mjini hapa. Lowassa ambaye pia amewahi kuwa Waziri Mkuu, alifika jana saa 2:40 katika viwanja vya Bunge na kutumia dakika kadhaa kusalimiana na baadhi ya wabunge nje ya ukumbi kabla hajaingia ndani. Alipoulizwa na gazeti hili kuhusu ujio wake bungeni, Lowassa, aliyekuwa Mbunge wa Monduli kwa tiketi ya CCM kwa takribani miaka 20 hadi...
Share:

nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba

nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba