Baraza
la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwaarifu Waombaji wote
walioomba kudahiliwa katika kozi za Astashahada (Cheti) na Stashahada
(Diploma) na Umma kwa ujumla kuwa dirisha la maombi lilifungwa mnamo
tarehe 15 Oktoba 2016 ili kuruhusu uteuzi wa awamu ya nne kwa waombaji
wa kozi hizo.
Uteuzi wa awamu ya nne kwa waombaji wa Astashahada na Stashahada unatarajiwa kutangazwa mnamo tarehe 2 Novemba 2016, hivyo basi waombaji wanaombwa kuwa na subira ili kutoa muda kwa Baraza kukamilisha taratibu za uteuzi huo.
Maombi mapya ya...
Thursday, 3 November 2016
Wednesday, 2 November 2016
Mke wa Lema aunganishwa kesi ya kumtusi RC Arusha
MKE wa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, Neema Lema
(33) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na kuunganishwa
katika kesi ya mume wake ya kumtukana Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho
Gambo kuwa ni shoga.
Akimsomea mashitaka hayo kwa mara ya kwanza, Wakili wa Serikali,
Blandina Msawa mbele ya Hakimu Augustino Rwezile, alidai kuwa kati ya
Agosti 20, mwaka huu ndani ya Arusha, Neema ambaye ni mkazi wa Njiro
alimtumia ujumbe wa simu ya kiganjani mkuu huyo wa mkoa wenye lugha ya
matusi, huku akijua ni kosa kisheria.
Alidai...
DC ataka Mwalimu Mkuu Mwananyamala kushushwa cheo
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji
wa Manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli kumshusha cheo Mwalimu Mkuu wa Shule
ya Msingi Mwananyamala B, Emmanuel Temba kwa makosa mbalimbali, ikiwemo
kufanya biashara shuleni.
Akitoa agizo hilo katika ziara ya kutembelea kata za manispaa hiyo
jana, Hapi alisema ametoa adhabu hiyo kwa kosa la kufanya biashara ya
vibanda shuleni hapo wakati agizo la serikali lililotolewa mwaka 2006,
haliruhusu biashara shuleni.
‘’Huyu mwalimu mkuu wa shule hii, hatufai haiwezekani afanye biashara
...
Watumishi changamkieni ununuzi wa nyumba-RC

WATUMISHI wa umma wameshauriwa kuchangamkia fursa ya kununua nyumba
zilizojengwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA) kabla ya muda wa kustaafu
ili kujitengenezea maisha mazuri baada ya kustaafu.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam, Paul Makonda wakati alipotembelea nyumba za watumishi
zilizojengwa na Wakala wa Majengo (TBA) zilizopo eneo la Bunju na nyumba
za wananchi Magomeni Kota.
Makonda alisema watumishi...
Tanzania yaipa somo ICC kukabili mpasuko
WAKATI nchi kadhaa za Afrika zikionesha dalili za kutaka kujiengua
kutoka Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), Tanzania
imeishauri mahakama hiyo kukaa meza moja na nchi wanachama wa Mkataba wa
Roma, hasa za Afrika ili kutafuta suluhu ya changamoto na tofauti
zilizopo kati ya mahakama hiyo na wanachama wake.
Imetoa mwito huo mwanzoni mwa wiki hii kupitia Mwakilishi wake wa
Kudumu katika Umoja wa Mataifa (UN), Balozi Tuvako Manongi wakati Baraza
Kuu la Umoja wa Mataifa lilipopokea na kujadili taarifa ya utendaji wa
ICC. Alisema...
Shein ahimiza mikutano ya watendaji kutatua kero

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed
Shein ameeleza umuhimu wa viongozi katika Ofisi na Idara za Serikali
kuwa na utaratibu wa kufanya mikutano mara kwa mara na watendaji wao ili
kuzungumza na kujadili masuala yao ya kazi.
Dk Shein aliyasema kuwa hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kujua
matatizo ya watendaji wao pamoja na kukaa kwa pamoja kwa lengo la
kujadili na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizopo...
Songwe wakamata mbegu feki za mahindi

POLISI katika Mkoa wa Songwe wamekamata kilogramu 455 za mbegu
zinazoaminika kuwa feki za mahindi katika msako mkali unaoendelea kwa
ushirikiano na Kampuni ya Mbegu ya Pana.
Kadhalika, watu watano wanashikiliwa na Polisi kutokana na
kujihusisha na biashara hiyo ya kuuza mbegu hizo na uchunguzi dhidi yao
unaendelea kufanyika.
Miongoni mwa maeneo ambayo msako umeendeshwa ni Mji Mdogo wa Mlowo
wilayani Mbozi ambako ndiko zimekamatwa mbegu...
Uvuvi haramu ‘huyeyusha’ matumbawe

MAKAMU wa Rais mstaafu, Dk Mohammed Gharib Bilal ameonya kuwa uvuvi
wa haramu unaofanywa na wavuvi katika maeneo ya pwani ya bahari ya Hindi
unatishia kutoweka kwa matumbawe, jambo ambalo lina madhara makubwa ya
kimazingira kwa nchi.
Akitoa mhadhara katika kongamano la mazingira na mabadiliko ya
tabianchi lililoandaliwa na kigoda cha Mwalimu Nyerere cha Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam, Dk Bilal alisema kitendo cha kuendesha uvuvi haramu
kunaharibu...
Mashali kuagwa Leaders leo

MWILI wa bondia wa ndondi za kulipwa nchini, Thomas Mashali aliyeuawa
Kimara jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Jumatatu, utazikwa leo
kwenye makaburi ya Kinondoni.
Baba mzazi wa marehemu, Malifedha Mashali alisema kuwa mwili wa mtoto
wake huyo aliyeuawa kwa kupigwa na watu wasiojulikana, utazikwa katika
makaburi ya Kinondoni Mwembejini.
Alisema mipango mingine ya mahali utakapoagiwa mwili huo na
utakapoombewa, bado ilikuwa inaendelea...
MNH wakusanya bil 4.6/- kwa mwezi
HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) imekuwa ikikusanya mapato ya Sh
bilioni 4.6 kwa mwezi kuanzia Desemba mwaka jana hadi kufikia Oktoba
mwaka huu, ikiwa ni ongezeko la asilimia 100.
Fedha ni zaidi ya wastani wa Sh bilioni 2.3 ilizokuwa ikizalishwa na
hospitali hiyo kwa kipindi kama hicho kuanzia Dasemba 2014 hadi Oktoba
2015.
Sambamba na ongezeko hilo, pia huduma za vipimo vya MRI, CT –Scan,
X-Ray na Ultra Sound zimeongezeka ambapo katika kipindi cha mwaka mmoja
sasa, jumla ya wagonjwa waliopimwa kwa kutumia vipimo hivyo wamefikia
55,073...
Serikali kutumia trilioni 32.9/- mwaka 2017/2018

SERIKALI imepanga kutumia Sh trilioni 32.946 katika bajeti yake ya
mwaka 2017/2018, ikiwa imeongezeka kutoka Sh trilioni 29.5 ya mwaka
2016/2017 na kutaja maeneo ya kipaumbele kuwa ni pamoja na kuzingatia
miradi ya kufufua kiwanda cha General Tyre cha Arusha na kuendeleza
maeneo ya viwanda vidogo.
Sambamba na hilo, serikali imebainisha mikakati yake ya kudhibiti
matumizi, ambapo sasa itahakikisha mikataba inayoingiwa na serikali na
taasisi...
Vyuo vikuu 15 kitanzini

SERIKALI imetoa siku mbili kwa vyuo vikuu 15, kuwasilisha matokeo ya
mitihani kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ya wanafunzi wanufaika na mikopo
wanaoendelea na masomo ili kupangiwa mikopo kwa mwaka wa 2016/2017.
Vyuo hivyo vilivyokuwa viwasilishe matokeo hayo siku 30 kabla ya
kufunguliwa, vimepewa siku hizo kuanzia jana, kabla serikali haijachukua
hatua zozote.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya
Ufundi, Maimuna...
Wapinzani wapinga takwimu ukuaji uchumi
LICHA ya takwimu za hivi karibuni kuonesha uchumi wa Taifa pamoja na
Pato la Taifa vimekuwa vikikua kwa kasi na kuifanya Tanzania kuwa moja
ya nchi zenye uchumi imara, kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imedai kuwa
uchumi wa Tanzania umeyumba.
Kambi hiyo imetaja baadhi ya maeneo yanayothibitisha hilo kuwa ni
mikopo inayotolewa na benki za biashara kwenye sekta binafsi kuwa
imeshuka katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016.
Waziri Kivuli wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Halima Mdee alisema
mikopo hiyo imefikia Sh bilioni 1,167.2 ikilinganishwa na...
Lowassa aongoza vigogo Chadema kuzuru bungeni
VIONGOZI wa juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
akiwemo aliyekuwa mgombea wa urais wa chama hicho, Edward Lowassa jana
walitembelea bungeni mjini hapa.
Lowassa ambaye pia amewahi kuwa Waziri Mkuu, alifika jana saa 2:40
katika viwanja vya Bunge na kutumia dakika kadhaa kusalimiana na baadhi
ya wabunge nje ya ukumbi kabla hajaingia ndani.
Alipoulizwa na gazeti hili kuhusu ujio wake bungeni, Lowassa,
aliyekuwa Mbunge wa Monduli kwa tiketi ya CCM kwa takribani miaka 20
hadi...