Thursday, 27 October 2016

UTOAJI WA MIKOPO KWA WANAFUNZI MWAKA 2016/2017

Baada ya kukamilisha zoezi la Uchambuzi wa maombi ya Mikopo 88,163 yaliyopokelewa hadi kufikia tarehe 11 Agosti, 2016. Jumla ya Wanafunzi wapya 20,183 wamepangiwa Mikopo. Upangaji huu umezingatia vigezo vilivyomo katika mwongozo wa  utoaji wa mikopo uliopitishwa na Bodi ya wakurgezi na kuidhinishwa na wizaya ya elimu sayannsi na teknoloji. Vigezo hivyo ni pamoja na:
 I. Vipaumbele vya  kitaifa vinavyoendana na Mpango  wa Maendeleo  wa Taifa wa Miaka mitano, Dira ya Taifa ya  Maendeleo 2025 na Mafunzo ambayo yatazalisha wataalamu wanaokidhi mahitaji  ya kitaifa katika fani za kipaumbele ambazo ni;
• Fani za Sayansi za Tiba na Afya,
• Ualimu wa Sayansi na Hisabati,
• Uhandisi wa  Viwanda, Kilimo, Mifugo, Mafuta na Gesi Asilia,
• Sayansi Asilia, na
• Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.
i. Uhitaji wa waombaji hususani wenye mahitaji  maalum kama vile ulemavu na uyatima
ii. Uhitaji wa waombaji wanaotoka katika familia zenye hali duni ya kimaisha
o Wadahiliwa yatima waliopata mkopo                                                 873
o Wadahiliwa wenye ulemavu wa  viungo                                             118
o Wadahiliwa  wahitaji wenye  mzazi mmoja                                      3,448
o Wadahiliwa wahitaji waliofadhiliwa na taasisis mbali mbali                     87
o Wadahiliwa wahitaji wanaosoma  kozi  za kipaumbele                      6,159
o Wadahiliwa wahitaji wanaosoma kozi zingine                                  9,867
Jumla                                                                                             20,183
Kiasi cha Fedha zinazohitajika
Bajeti iliyoidhinishwa kwa ajili ya ukopeshaji kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 ni shilingi bilioni 483, kwa ajili ya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza wapatao 25,717, na wanaoendelea na masomo wapatao 93, 295.
Hatua zinazofuata
I. Wanufaika wote wanaopungukiwa na sifa watachunguzwa kwa ajili ya kurekebishiwa au kuondolewa katika unufaika wa mkopo
II. Waombaji waliwasilisha taarifa zenye upungufu, taarifa zao zitahakikiwa, na wakibainika kuwasilisha taarifa za uongo watachukuiwa hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kufutiwa mikopo yao
III. Wanufaika wote watatakiwa kuhuisha taarifa kwa kujaza dodoso. Taarifa za ziada za kiuchumi za wazazi au walezi wao zitatumika kutanua uhalisia. Wale watakaokutwa na hadhi zisizo stahili, watapoteza sifa za kuendelea kupata mikopo na kulazimika kurejesha kiasi watakachokuwa wamepokea tayari.
IMETOLEWA NA:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Share:

Majibu ya Meya Kinondoni kwa wanaohoji uwepo wa Dk. Tulia na Ndalichako

Share:

Baada ya Mchungaji Lwakatare kuwatoa wafungwa DSM, sasa ni zamu ya Dodoma


Ikiwa siku kadhaa zimepita tangu Mchungaji wa Kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni B, Dk. Getrude Lwakatare kutoa milioni 25 kwa ajili ya kuwalipia wafungwa 78 ambao walikosa fedha za kulipia faini na kufungwa jela mkoa wa Dar es salaam.  Sasa amejitolea kuwalipia faini wafungwa 50 walioko kwenye magereza mkoani DODOMA, wakiwemo wanaonyonyesha, wazee na watoto.
Akizungumza na Ayo Tv na millardayo.com, Lwakatare amesema …..>>>‘Siku ya ijumaa itakuwa kwa ajili ya Dodoma tumefanikiwa kuwalipia faini za watu wenye makosa madogo madogo ya elfu hamsini, ya laki na nusu kwa watu wapatao 50 na tulitoa kipaumbele kwa watu wanaonyonyesha watoto, wagonjwa, wazee vikongwe, wale watu ukiwalipia unapata thawabu kwa Mungu’
Share:

Mabadiliko ya Yanga na Simba yapigwa stop na serikali

Serikali imezipiga stop klabu za Yanga na Simba kuendelea na michakato yao ya kubadili umiliki wake hadi pale yatakapofanyika marekebisho ya katiba zao.
YangaSimba
Hayo yalitangazwa jana na Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohamed Kiganja alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Hivi karibuni klabu hizo kongwe ziliazimia kuingia kwenye mabadiliko, Yanga ikikodishwa na mwenyekiti wake Yusuf Manji na Simba ikitaka kuuza hisa asilimia 51 kwa mfanyabiashara Mohamed Dewji ‘Mo’.
Kiganja alisema Serikali haikatai mabadiliko ya uendeshaji katika klabu hizo pamoja na nyingine za wanachama, ila inachotaka kwanza kufanyike marekebisho ya katiba zao kwani za sasa haziruhusu mabadiliko hayo.
Alisema kuwa BMT inapenda kuona wahusika wanafuata sheria na taratibu za nchi katika kufikia malengo yao, ambapo alisisitiza kuwa kuendelea na michakato hiyo kabla ya kurekebisha katiba zao ni kosa na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
“Hivi karibuni kumeibuka michakato ya watu wakitaka kubadilisha umiliki wa klabu za wanachama na kuzielekeza katika utaratibu wa hisa na ukodishwaji, vitendo vimesababisha migogoro mikubwa ambayo inaashiria uvunjifu wa amani…,” alisema.
Kiganja alisema tayari mezani kwake kuna barua nyingi za wanachama wa Yanga wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato huo wa kubadilisha umiliki.
Kwa mujibu wa katiba ya Yanga iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 Ibara ya 56 inaeleza kuhusu kampuni ya umma: Inaeleza kuwa kutakuwa na kampuni itakayojulikana kama Young African Sports Corporation Limited ambayo itasajiliwa chini ya sheria ya makampuni kama kampuni ya umma yenye hisa.
Sehemu ya pili ya ibara hiyo inasema wanachama wote katika klabu ambao katika tarehe ya marekebisho ya Katiba ya mwaka 2007 wako hai kwa nguvu ya uanachama wao watakuwa wanahisa katika kampuni kwa kiwango cha idadi ya hisa watakapopata kwa mujibu wa muafaka wa Yanga uliofikiwa na wana Yanga Juni 22, 2006.
Klabu itamiliki hisa zilizosawa na asilimia 51 ya hisa zote zilizomo katika klabu hiyo. Mkutano Mkuu wa Uchaguzi utachagua wanachama wawili, ambao sio miongoni mwa viongozi wa klabu kuwa wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni kwa ajili ya kuwakilisha maslahi ya klabu kwenye kampuni.
Tayari Yanga iko chini ya Kampuni ya Yanga Yetu ambayo ni mali ya mwenyekiti wa klabu hiyo Manji, ikiwa ni kinyume na katiba yao wenyewe.
Kiganja alisisitiza kuwa klabu zisitishe mipango ya kubadilisha uendeshaji na ziendelee kuwa mali ya wanachama. Wakati Yanga walikuwa tayari wameishaingia mkataba wa miaka 10 wa
kuikodisha klabu yao, wenzao wa Simba walijipa miezi sita kukamilisha taratibu za kuuza hisa.
Share:

Model anayedaiwa kutoka kimapenzi na Wema na kudai hamjui Idris Sultan anyoosha maelezo

Wiki moja iliyopita kupitia kipindi kimoja cha runinga, model huyo alisema hamjui Idris Sultan.
Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Calisah alisema ni kweli kwamba hamjui Idris Sultan na wala hakuongea kwa nia mbaya au kutafuta kiki.
“Mimi nashangaa kwanini watu wamepanic kisa kusema simjui Idris Sultan, kwani yeye ni nani kila mtu amjue?,” aliuliza Model huyo. “Wewe kuna wanamichezo wangapi wameshachukua tuzo kubwa duniani hawajui?. Kwahiyo mimi nadhani watu ambao wananishambulia katika mitandao hawajui nini wanafanya,”
Aliongeza,”Sikusema hivyo kuonyesha dharau, kwa sababu nipo karibu na Wema lakini hajawai kuniambia kuhusu mtu kama huyo na sijawahi kumuona naye, na kama ukiwa na mwanamke halafu akawa azungumzia mwanaume mwingine hizo ni dharau sana. Kwahiyo kiukweli mimi jamaa nimeanza kumjua baada ya watu kinitag picha zake katika mitandao ya kijamii,”
Pia model huyo alisema kwa sasa hawezi kuweka wazi kama ni kweli anatoka kimapenzi na Wema Sepetu huku akidai Wema ndiye atayekuwa na jibu sahihi juu yake.
Share:

Dayna Nyange: Lebo yoyote itakayokubali masharti yangu nitafanya nayo kazi

Hitmaker huyo wa ‘Komela’ amemuambia mtangazaji wa Maisha FM ya Dodoma, Silver Touchez “Kikubwa nachoangalia ni sababu, kabla sijajiunga na lebo yoyote lazima niwe na vitu vyangu ambavyo navitaka na wao wanavitu vyao wanavyotaka.”
“Record label ni studio tu ambao watu watakuwa wanasimamia kazi zangu ni kitu ambacho mimi mwenyewe ninaweza nikaenda sehemu yoyote nikafanya kazi zangu. Kuna vitu vingi sana kabla hujaingia kwenye lebo yoyote kama kuna makubaliano mazuri yatakuwepo basi tutafanya kazi,” ameongeza.
Katika hatua nyingine muimbaji huyo amekanusha kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na Idris Sultan zaidi ya kuwa marafiki tu.
Share:

Man Utd kukutana na West Ham robo fainali EFL Cup

Mechi za robo fainali EFL Cup ratiba imetoka baada ya kumuondoa Guardiola, Mourinho sasa atacheza na Bilic.
Mechi hizi zitachezwa katika wiki inayoanza Tarehe 28,Novemba.
Hii ndo ratiba kamili ya Michuano ya EFL Cup.
Share:

‘Magufuli ameletea msiba Dodoma’

WAKATI serikali ya awamu ya tano ikiendelea na hekaheka za kuhamishia makao makuu yake mkoani Dodoma, baadhi ya wakazi wa mkoa huo wamelaani hatua hiyo ya serikali na kusema inawasababishia matatizo makubwa,

Wakizungumza na mtandao huu, wakazi wa Ndachi kata ya Miyuji, Manispaa ya Dodoma, wamesema baada ya serikali kutangaza kuhamishia makao makuu yake Dodoma, tayari wameanza kuporwa ardhi yao.
Wameenda mbali zaidi na kutishia kuwakata kwa mapanga na kuwajeruhi kwa mishale watu wanaovamia maeneo yao kwa madai kuwa wana hatimiliki kutoka Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) pamoja na halmashauri.
“Sisi tunafahamu kuwa eneo hili halijapimwa na watu tuliopo hapa ni wazawa hivyo tunashangazwa na watu kuja na kudai wana hatimiliki za maeneo haya.
“Tunajutia uamuzi wa Rais Magufuli kuhamishia rasmi makao makuu ya nchi Dodoma, tumeanza kupata matatizo makubwa, watu wenye hati wanadai kuwa wameuziwa maeneo yetu,” amesema Nicholaus Lupimo, Mkazi wa Ndachi.
Ameongeza kuwa, wamekuwa wakipigwa na askari walioagizwa kuondoa wazawa, ambao wanaitwa wavamizi katika eneo hilo licha ya kuishi hapo kwa zaidi ya miaka hamsini sasa.
John Masala, aliyezaliwa mwaka 1954 katika eneo la Ndachi amesema Babu na Baba yake wamekuwa wakazi wa eneo hilo tangu mwaka 1915 na kwamba hata yeye alizaliwa katika eneo hilo ambalo ameishi mpaka sasa.
“Sisi hatujatoka Rwanda wala Burundi, kama wanatuona sisi ni wakimbizi au wavamizi basi waturudishe tulipotoka,” amesema.
Kwa upande wake Jackson Mpilimi, ameeleza kuwa alizaliwa katika eneo hilo mwaka 1968, na hawajawahi kuhama wala kuona maeneo hayo yanapimwa katika kipindi chote hicho.
“Baada ya tangazo la Serikali kuhamia rasmi Dodoma, watu wameingia katika eneo hili wakiwa na hati tunazoamini kuwa ni ‘feki’ wanadai kuwa walishauziwa maeneo haya. Tunafukuzwa na polisi na kupigwa mabomu,” amesema.
Wananchi hao waliamua kuitisha mkutano wa hadhara baina yao na Godwine Kunambi, Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma siku ya leo ambapo alifika katika eneo hilo ili kusikiliza madai yao.
Amewaomba wananchi hao kumpa siku saba ili aweze kufuatilia kwa kina na kujua kama eneo hilo kama lipo chini CDA au manispaa.
“Nawaomba muwe watulivu nitashughulikia jambo hili ndani ya siku saba na kuwapatia majibu ya kina. Hakuna haki ya mtu yeyote itakayopotea, kama kuna watendaji au mamlaka imehusika katika kupoteza haki za wananchi basi tutatoa taarifa sehemu husika na hatua zitachukuliwa,” amesema.
Share:

RC MWANZA APOKEA UJUMBE WA WAWEKEZAJI KUTOKA KOREA.

  • Awaahidi ushirikiano.
  • Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amepokea ujumbe wa wawekezaji kutoka nchini Korea Kusini, wenye niya yakuwekeza katika mkoa wa Mwanza ukiwa na ujumbe wa watu kumi na watano nakufanya nao mazungumzo mapema katika Ofisi yake kabla yakuendelea na ziara yao katika Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.
    Katika mazungumzo yao yaliyodumu saa 1:33, Mkuu wa Mkoa amewahakikishia utayari wa mkoa wa Mwanza kuwapokea wawekezaji kutoka nchini humo lakini pia kuwabainishia maeneo mbali mbali katika sekta ya uchumi ambayo watu wa Korea kusini wanaweza kuwekeza.
    Alianza kwakuwashukuru sana kwakutambua urafiki wa nchi hizi mbili ambao umeanza miaka ya 1960’s, na kuwaambia kuwa Mwanza ni mkoa ambao una fursa nyingi za uwekezaji katika Nyanja mbali mbali ikiwapo: Viwanda, Biashara, Kilimo, uvuvi, Mifugo, kwakutaja baadhi.
    Mkuu huyo wa mkoa ameuwambia ujumbe huo wa watu wa jamhuri ya Korea kusini, uliokuwa unaomngozwa na Bw. Son Yang Soo, kuwa Mwanza ndio sehemu pekeee katika nchi za eneo la maziwa makuu inayo liunganisha soko la Afrika Mashariki kwa nchi za South Sudan, Rwanda, Burudi, Jamhuri ya Congo na hata Kenya na Uganda
    Mkuu wa mkoa amesema kutoka na uchumi wa Mkoa wa Mwanza kufikia Tril. 8.45 kwa mwaka katika uzalishaji lakini pia Mwanza ndio mkoa unaochangia pato la Taifa ukishika nafasi ya pili ambapo mchango wake ni asilimia 9.4 katika pato la taifa ukitanguliwa na Dar es Salaam unaochangia kwa asilimia 17 kwa mwaka, hivyo kwa watu wanaotaka kuwekeza Mwanza wamewaza vyema kama jinsi ujumbe huu wa Korea Kusini ulivyo fanya.
    Naye kiongozi wa msafara huo, Song Young Soo, alianza kwakuwapa Watanzania pole kufuatia tetemeko la Ardhi lililotokea tarehe 10, Septemba na kuathiri zaidi Mkoa wa Kagera na mara baada ya hapo, akasema wamefurahishwa na jitihada zinazo chukuliwa na mamlaka ya serikali katika kuahakikisha wawekezaji wanapata fursa yakuwekeza, Song amesema katika Nchi ya Korea Kusini uwekezaji umejikita katika nyanja za Teknolojia ya habari na mawasiliano, Afya na Viwanda kwa ujumla, aidha amesema kufuatia ziara iliyofanywa na mbunge wa Ilemela na Ujumbe wake mapema Mwaka huu, hiyo sasa imeibua chachu na muendelezo wa ushirikiano wanachi wanchi hizi mbili ambazo zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu sasa.
    Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makaazi Dkt. Angeline Mabula (MB), amewataka wana watanzania na wana Mwanza kwa ujumla wao , kuonesha utayari na kuwapokea wageni wanao kuja kwa nia njema yakuwekeza katika Mkoa wa Mwanza “ Niwa ombe tuu wananchi wa Tanzania, kuonesha utayari wakupokea wawekezaji, tunaimba viwanda, viwanda vikiwapo watakao ajiriwa ni watanzania wenye sifa husika, hivyo nilazima tunapopata wawekezaji tuwe na utayari na ukarimu kwa wageni wetu hasa wawekezaji wema na kuwapa ushirikiano kwenye maeneo yetu,” alisema Mabula.
    Ujumbe huo wa Korea Kusini ulikuwa ukiongozwa na Song Yaung Soo, wajumbe wengine ni Shing Jong Sam, Cho Yoop Gon, Kim Gi Geob, Doewak Kim, KTM Kyu il, wengine ni Rark in Nwan, Kim Il Hyun, Kim Ji Mi, Lee Suk Hoom, Kim Chan Kyu, Byun Kyumg Ho, Lee Joom Hwa na Kim Lim Gon na Mkalimani wao aliyekuwa anaitwa Alex Gang.
    Ujumbe huo wa Korea pamoja na mambo mengine utatembelea eneo la Nyamongholo kisha utapata fursa yakujionea Matayarisho ya Mpango Kamambe ya urasimishaji wa Makaazi ya Jiji la Mwanza na mpangilio wake.
    Share:

    RC MWANZA ATOA SOMO KWA WAREMBO MISS TANZANIA. 2016

    MKUU wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, amewaasa warembo wanaoshiriki shindano la Mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania-2016), kutambua wana jukumu zito mbele yao la kuzisaidia jamii zao katika majukumu mbali mbali ya kijamii.
    Mongella alitoa kauli hiyo muda mfupi mara baada ya warembo 30 wanaoshiriki shindano hilo kumtembelea ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha.
    Mongella aliwataka warembo hao kufanyakazi kwa bidii na kujituma kwani ndio njia pekee itakayowawezesha kuondokana na umasikini.
    “Jijengeeni tabia yakufanyakazi kwa bidii na maarifa tena bila kuchoka, hii awamu ya tano ni awamu ya hapa kazi tuu, hivyo kama warembo mnalo jukumu zito la kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais katika kufanya kazi na hasa katika kazi za kijamii, lakini haya yote yatawezekana mkiwa wadilifu na wachapa kazi, sasa hivi mpo kwenye U miss wewe pambana na jenga tabia yakufanya kazi masuala ya nani atakuwa mshindi waachie majaji, alisema Mongella.
    Katika hatua nyingine Mongella amewashauri warembo hao kuto ionea haya Lugha ya Taifa ya Kiswahili, k wakuwa fikra sahihi huja kwa lugha sahihi, amewataka kuinze Lugha hiyo wakati wa mashindano hasa pale wanapotakiwa kujieleza ili kuweza kufikisha ujumbe kwa jamii kwa wepesi.
    Akizungumza kabla yakumkaribisha mkuu wa mkoa wa Mwanza, mmoja wa waratibu wa Mashindano hayo Bibi Pamella Irengo, amesema, wamefurahi sana kama mkoa wa Mwanza kuyapokea mashindano hayo, kwani hii ni mara ya kwanza mashindano hayo yatafanyika nje ya mkoa wa Dar es salaam.
    “Mhe. Mkuu wa Mkoa mashindano haya kwa miaka 21, yamekuwa yakifanyika Mkoa wa Dar es salaam, hivyo kuyaleta Mwanza sisi kwetu ni fursa ya kipekee katika kuutangaza mkoa wetu lakini tunashukuru sana uongozi wa mkoa kwakutuunga mkono nakutupokea kwa moyo mkunjufu.
    Mashindano ya kumsaka Mrembo wa Tanzania yatafanyika Oktoba, 29, 2016 katika Ukumbi wa Rock City Mall, ambapo warembo wapatao thelasini (30), watachuana kumsaka mrembo mmoja atakaye peperusha Bendera ya Taifa katika mashindano ya Dunia na Kauli mbiu ya mashindano hayo kwa Mwaka huu ni
    “Mrembo na Mazingira safi”.
    Share:

    Ofisa usalama feki atupwa jela miaka 2

    MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala imemhukumu Seleman Manoti, kifungo cha miaka miwili jela kwa kupatikana na hatia ya kujifanya usalama wa Taifa.
    Hata hivyo, mahakama imetoa hukumu hiyo bila mshitakiwa kuwepo mahakamani kutokana na kuruka dhamana kesi hiyo ilipokuwa inasikilizwa.
    Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi, Flora Haule alisema kuwa upande wa mashitaka, ulileta mashahidi wanne kwa ajili ya kuthibitisha tuhuma hizo.
    Alisema kutokana na ushahidi uliotolewa, mahakama imeridhishwa na ushahidi huo na kwamba mahakama inamtia hatiani mshitakiwa licha ya yeye kutokuwepo.
    “Hati ya kumkamata mshitakiwa itolewe na adhabu hii itaanza kutumika pindi mshitakiwa atakapokamatwa kwani alitoroka akiwa na haki ya kusikilizwa,” alisema Hakimu Haule.
    Wakili wa Serikali, Ester Kyara aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa iwe fundisho kwa wengine.
    Inadaiwa kuwa Novemba 19, 2014 maeneo ya Kariakoo Msimbazi wilayani Ilala, mshitakiwa alijitambulisha kwa Issaya Odelo na Charles Odinga kuwa Ofisa Usalama wa Taifa, kitu ambacho alijua si kweli. Katika hatua nyingine, kondakta Ally Salum (23), mkazi wa Mwananyamala, amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kuiba daladala.
    Mbali na mshitakiwa huyo, Exavery Kaunga (44) ambaye ni mlinzi na mkazi wa Kiwalani, Minazi Mirefu, aliachiwa baada ya ushahidi dhidi yake kuwa na shaka.
    Akitoa hukumu hiyo jana katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Hakimu Mkazi Mwandamizi, Juma Hassan, alisema kuwa upande wa mashitaka ulileta mashahidi wanne kuthibitisha kosa hilo.
    “Nimeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka, nakutia hatiani mshitakiwa kama ulivyoshitakiwa kwa kutumikia kifungo cha miaka mitano jela,” alisema Hakimu Hassan.
    Kabla ya kutolewa adhabu hiyo, Wakili wa Serikali, Grace Mwanga aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwa wengine. Hata hivyo, mshitakiwa alipoulizwa ni kwa nini asipewe adhabu kali, hakujibu chochote na mahakama kutoa adhabu hiyo.
    Washitakiwa hao walishitakiwa kwa makosa mawili ya kula njama kutenda kosa ambapo inadaiwa kati ya Julai 5, mwaka jana, washitakiwa walikula njama kutenda kosa.
    Pia inadaiwa Julai 5,2015 pembezoni mwa barabara ya Nyerere katika Kituo cha Mafuta cha Victoria, washitakiwa waliiba gari lenye namba za usajili T 624 CSH aina ya Eicher mali ya Kampuni ya White Swan.
    Share:

    nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba

    nunua vitabu vya watoto kuanzia chekechekea mpaka darasa la saba